🚨 JUST IN: Kocha mkuu wa Simba, Abdelhak Benchikha amerejea nchini kutoka kwenye mafunzo ya siku tano ya kuongeza ujuzi alionao, huku akitoa kauli inayoweza kuwapa mzuka mashabiki wa klabu hiyo, kwa kusema licha ya kupangwa na watetezi wa Ligi ya Mabingwa Afrika, Al Ahly ya Misri, hana presha nao kwa vile wanaijua na kwamba watakula nayo sahani moja.
.
“Ahly wanajua kuwa wanakwenda kukutana na mpinzani mgumu kwa kiasi gani na Simba itakwenda kupigania nafasi ya kwenda nusu fainali na sio kuhofia hadhi yao. Tunatakiwa kujipanga kwenda kuthibit-isha kwanini tupo kwenye klabu kumi bora Afrika kwa kushindana na klabu namba moja na bila hofu kila kitu kinawezekana,” alisema Benchikha.
Tembelea
@kick_offnews